Pembetatu mraba

Kutoka testwiki
Nenda kwa urambazaji Nenda kwa kutafuta
Pembetatu mraba

Pembetatu mraba ni aina ya pekee ya pembetatu yenye pembe moja ya nyuzi 90°. Pembe mbili nyingine zina jumla ya nyuzi 90°.

Pande zina majina maalumu kutokana na kawaida ya wanahisabati ya Ugiriki wa Kale.

  • Pande ndefu kinyume cha pembe mraba ni hipotenusi au kiegana.
  • Pande mbili nyingine zinazoanza kwenye pembe mraba huitwa miguu au kwa neno la Kigiriki katheti.


Tabia za pembetatu mraba yenye hipotenusi c
Majina ya pande a,b,c
majina ya pembe α,β,γ=90
kimo h=abc
eneo A=ab2
mzingo U=a+b+c


  • uhakiki wa Thales husema kila pembetatu ambayo kona zake ziko kwenye nusuduara sharti ni pembetatu mraba.
  • uhakiki wa Pythagoras husema ya kwaba mraba juu ya hipotenusi ni sawa na jumla ya miraba juu ya miguu (katheti).


Kigezo:Mbegu-sayansi