Uzidishaji

Kutoka testwiki
Nenda kwa urambazaji Nenda kwa kutafuta
Alama ya uzidishaji.

Katika hisabati, uzidishaji (kwa Kiingereza: multiplication) ni mojawapo kati ya vitendaji vinne vya hesabu(pamoja na ujumlishaji, utoaji na ugawanyaji). Uzidishaji ni kinyume cha ugawanyaji. Alama ya uzidishaji ni Kigezo:Char.[1][2]

Mfano wa 3 × 4 = 12 magololi.

Kwa usahihi, uzidishaji ni tendo la kujumlisha namba fulani mara kadhaa. Kwa mfano:

3×4=3+3+3+3=12.

Katika mlinganyo huu, 3 ni kizidishi, 4 ni kizidishio na 12 ni zao. Kizidishi na kizidishio ni vigawo vya zao. Hata hivyo, mpangilio wa kizidishi na kizidishio haubadilishi zao. Yaani:

4×3=4+4+4=12.

Kanuni hii hujulikana kama tabia ya mabadiliko ya kuzidisha.

Marejeo

Kigezo:Marejeo Kigezo:Mbegu-hisabati